Ijumaa, 21 Februari 2020

MAJERUHI PEKEE ALIYE BAKI SIMBA (MILAJI)

Baada ya Mzamiru Yassin kuanza mazoezi hapo jana, Miraji Athumani ndiye mchezaji pekee ambaye anaendelea kuwa nje ya dimba akiuguza majeraha

Miraji amekuwa nje kwa takribani miezi miwili sasa akiuguza majeraha hayo ya goti

Kabla ya kupata majeraha, Miraji alikuwa kwenye kiwango bora akifunga mabao sita

Pamoja na kukosekana kwake Simba imeendelea kufanya vizuri kutokana na ubora wa kikosi chake

Deo Kanda ni mchezaji mwingine aliyekuwa majeruhi lakini tayari amerejea kikosini

LUGORA NA ANDENGENYE WAKUTWA NA MAKOSA

  LUGOLA NA ANDENGENYE WAKUTWA NA MAKOSA

Taasisi ya kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini TAKUKURU imesema uchunguzi wa sakata la manunuzi ya vifaa vya zimamoto na uokoaji yasiyozingatia sheria na taratibu za nchi ambao ulisimamiwa na aliyekuwa Waziri wa mambo ya ndani KANGI LUGOLA na aliyekuwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto THOBIASY ANDENGENYE umekamilika kwa asilimia 99.9

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Brig. Jenerali John Mbungo, ameviambia vyombo vya habari kuwa uchunguzi umebaini makosa mengi katika mkataba wa manunuzi hayo ambayo kwa pamoja yanatengeneza kosa la uhujumu uchumi.

Baada ya kukamilika kwa uchunguzi huo TAKUKURU wanapeleka taarifa ya uchunguzi huo kwa Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali tayari kwa hatua za kisheria ikiwemo kuwafikisha mahakamani watuhumiwa wote 17 wa sakata hilo.

NINI MAONI YAKO Usisahau KU-LIKE na KU-SHARE ukurasa wetu ili uwe karibu na habari zote pindi zinapochipuka.

Jumamosi, 15 Februari 2020

Alhamisi, 9 Januari 2020

NDEGE KUBWA DUNIANI KOTE HII HAPA

   
            By zakaboyblog
   Kwa matangazo wasiliana nasi                  076620224

Jumatano, 8 Januari 2020

IRAN YAUA WAMAREKANI 80 (VITA KUU YA 3)

Televisheni ya taifa la Iran yatangaza kuwa Wamarekani 80 wameuawa, baada ya Iran kushambulia kambi mbili za jeshi la Marekani nchini Iraq kwa makombora zaidi ya 10.

Vifo Marekani vyaongezeka kutokana na ulevi

UTAFITI MAREKANI: VIFO VITOKANAVYO NA ULEVI VYAONGEZEKA MARA 2

> Kulingana na uchambuzi mpya wa vyeti vya kifo, vifo vinavyohusiana na unywaji wa pombe kwa watu wenye umri wa miaka 16 na zaidi vimeongezeka kutoka vifo 35,914 mwaka 1999 hadi kufikia vifo 72,558 mwaka 2017

> Wanaofariki sana ni wanaume wenye umri wa kati huku wanawake nao wakishika kasi ktk utumiaji vilevi

S

Jumatatu, 6 Januari 2020

Marubani wa Ndege za Kivita Za Iran wakiwa mguu sawa

Marubani wa Ndege za Kivita Za Iran wakiwa mguu sawa kuanza kurusha Ndege endapo Kiongozi ataamuru Kuishambulia Marekani. #zakaboyblog
Kwa tangazo
0766620224

Uchawi wa mashabiki wa simba taifa

     
     By zakaboyblog
    Namba ya matangazo 
         0766620224

KATIKA SAFARI YA MAISHA KUELEKEA MAFANIKIO MAMBO HAYA HAYAEPUKIKI UTAYAKUTA TYU

Ni kwamba kama unahitaji kufanikiwa lazima ujifunze kudili
na kukataliwa (rejection)

Katika maisha yako lazima itatokea watu wakakukataa kabisa. Marafiki watakukataa, wafanyakazi wenzako watakukataa, maombi yako ya kazi yatakataliwa, wateja wa kununua bidhaa zako watazikataa.

Na zaidi Mpenzi uliemwamini ukampa kila kitu, ukajishusha kwake na kukubali kuwa mtumwa wake atakukataa.

Lakini kama unayo kiu ya mafanikio na unahitaji kufanikiwa lazima ujifunze kudili na huko kukataliwa na kusonga mbele kwa ujasiri mkubwa(ku-move on great passion!)

Hauwezi ukaendelea kuishi maisha ya huzuni, majuto na hofu ya wale waliokukataa, waliokuacha katika wakati mbaya, waliokusaliti na waliokupotezea muda wakati ulikuwa sehemu ya mafanikio yao!

You have let go(Ni lazima uwaache waende) na ku-focus(ujikite) katika kutimiza kusudi la uwepo wako na punde kidogo waliokukataa watakuona uko kileleni(At the top!)

Yesu kristo mwenyewe alisema "Jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni" (I.e the stone which the builders rejected is put right at the Top)
Kubali kukataliwa na waashi, na muda si mrefu(soon) utakuwa jiwe kuu la pembeni linalokimbiliwa na si kukimbiwa!

Nilichojifunza kwa miaka yote hii ninayopitia magumu na changamoto fulani fulani katika maisha yangu kiujumla, ni kwamba MUNGU anayo tabia ya kuwabariki watu waliokataliwa.

Mungu anayo tabia ya kuwatumia wale watu waliodharauliwa hapo awali kutimiza lengo na kusudi lake,usiogope wewe ni mmoja wa wale waliokubaliwa na Mungu vya duniani visikupe presha na kukutoa kwenye uwepo na baraka za Mungu

DKT.LOUIS SHIKA(MIA TISA ITAPENDEZA ALAZWA



Mkazi wa jiji la Dar es Salaam Dkt.LOUIS SHIKA (Mia Tisa Itapendeza) moja ya watu wachache waliyojizolea umaarufu uliodumu kwa kipindi kifupi jijini Dar es salaam ,amelazwa katika hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala kwa matibabu.

Dkt. SHIKA ambaye katika siku za karibuni amekuwa akishinda na kulala katika maegesho ya magari katikati mwa jiji la Dar es salaam amelazwa katika hospitali hiyo kwa muda wa siku mbili sasa huku watu wake wakaribu wakisema bado hawajui anaugua ugonjwa gani

By zakaboyblog
 By #westzonetv
    0766620224

Jumatano, 16 Oktoba 2019

Matokeo ya darasa la saba shule ya msingi Kalenge


ANATAFUTA NDUGU ZAKE

Atafuta ndugu zangu nimepotezana nao toka mwezi wa sita nipo vijijini mkoani Shinyanga mwenye kunijua anitafute kwenye namba hii 0747507058

     BY ZAKABOYBLOG
     BY UWANJA WA NDUGU

KAMA UNA TABIA. HIZI MAFANIKIO KWAKO YATABAKI KUWA NDOTO

Adui wa kwanza wa mafanikio katika maisha yako ni wewe mwenyeweWewe ndiye unayeamua,ufanikiwe au usifanikiwe. Ninaposema hivi nina maana kwamba ziko tabia ambazo ukiwa nazo unafanikiwa na zipo tabia  mbazo ukiwa nazo utaishia kuona wenzako wanafanikiwa wewe unabaki palepale.Tabia hizi ni adui mkubwa wa mafanikio yako.Kwa hiyo usianze kutafuta mchawi wa mafanikio yako,mchawi wa kwanza niwewe. Wewe ndiye mwenye maamuzi ya mwisho juu ya maisha yako unataka yaweje.

Hizi ni tabia ambazo umekuwa nazo kwa muda mrefu na hutaki kuziachia. Kwa jinsi unavyoendelea kuwa nazo ndivyo ambapo unajikuta maisha yako yanazidi kuwa magumu na wakati huo huo mafanikio kwako yataishia kuwa ndoto ya saa sita mchana, ndoto ya alinacha na mara nyingi utajikuta ukiishi maisha ya wasiwasi huku ukiwa hauna uhuru katika maisha yako. Unapojifunza tabia hizi fanya mabadiliko, chukua hatua sahihi za kubadili maisha yako na utafanikiwa.

Hizi ndizo tabia ambazo ukiwa nazo, mafanikio kwako yataishia kuwa ndoto za mchana:-

1.Kutokuwa na malengo.
Ili mtu afanikiwe lazima awe na malengo.Malengo ndio chanzo cha mafanikio, mafanikio hayaji kwa bahatí mbaya. Watu wote waliofankiwa unaowafahamu na usiowafahamu walikuwa na malengo, wakayaweka katika vitendo na kufanikiwa. Kama wewe ni mwanafunzi weka lengo unataka kuwa nani baadaye, vinginevyo utaishia kusoma na kubaki huna kazi ya kufanya; unakuwa umepoteza muda bure katika maisha yako.

Kama wewe ni mfanyabiashara weka lengo la kuwa mfanyabiashara mkubwa. Zingatia kwamba malengo ndiyo yanakupa dira na muelekeo katika maisha yako. Kupitia malengo unajua unatakiwa uanzie wapi na uishie wapi kulingana na lengo ulilojiwekea kwa wakati huo. Kutokuwa na malengo katika maisha ni sawa sawa na kusafiri bila kujua unaenda wapi. Hii ni hatari sana kwako.

By zakaboyblog 0763230371


2 .Kutokuwa na malengo  maalum yanayoeleweka.
Kuwa na malengo haitoshi, ni lazima uwe na malengo yanayoeleweka na kufikika. Ni kosa Kubwa kuwa na malengo mengi Ambayo hayafikiki na kutaka kuyatekeleza kwa wakati mmoja. Kuwa na malengo mengi  humfanya mtu achanganyikiwe. Mtu mwenye malengo mengi ana hatari ya; Kuchanganyikiwa na kushindwa kuamua aanze na lipi, amalize na lipi,pia ana hatari ya kutekeleza mambo nusunusu na hatimaye kushindwa kuendelea kabisa na mipango hiyo.

Weka malengo machache ambayo una uwezo wa kuyatekeleza kwa muda uliopanga kisha anza kutekeleza mpango mmoja hadi mwingine. Ukishafanikiwa kutekeleza mipango hiyo weka lengo lingine na utazidi kupiga hatua moja hadi nyingine na kuzidi kufanikiwa siku hadi siku.

3. Kukosa uvumilivu.
Mafanikio ni safari ndefu sana katika maisha ya binadamu. Mafanikio ya kweli yanachukua muda mrefu kupatikana, hayachukui muda mfupi kama wengi tunavyotaka. Kutaka mafanikio kwa muda mfupi ni tatizo ambalo limetukumba wengi katika dunia ya leo yenye changamoto nyingi za kiuchumi, kijamii na kisiasa. Watu wengi tunaiogopa safari ndefu ya mafanikio, tunataka mafanikio ya muda mfupi.

WatuWengi wanakata tamaa mapema kwa kwa sababu wanataka mafanikio kwa mnuda mfupi jambo ambalo haliwezekani. Matokeo yake wanaamua kupita njia za mkato ili kufikia malengo wanayojiwekea. Usiogope kuchukua muda mrefu hadi kufanikiwa,hayo ndiyo mafanikio ya kweli. Ikiwa unataka kufikiamafanikio, usiogope kupita jangwani.

Jumanne, 8 Oktoba 2019

Mkazi wa kijiji cha Kalenge abaka mtoto

Mkazi wa Kijiji cha Kalenge, wilayani Uvinza, Dastani Elia (40), akiwa chini ya ulinzi wa Askari Polisi baada ya kufikishwa katika Mahakama ya Wilaya Mkoa wa Kigoma jana na kusomewa mashtaka ya kumbaka mtoto wa kike mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi 7 na kumsababishia maumivu makali sehemu zake za siri.

Jumatano, 28 Agosti 2019

Sikiliza na tazama video ya asray chuki

   

                           By ZAKABOYBLOG
Waweza tuma tangazo lako kupitia         
                           "no"0763230371

Ijumaa, 9 Agosti 2019

WAJIBU WA SERIKALI KWA WANANCHI WAKE

Habari rafiki msomaji wa mtandao huu,
Leo napenda tujifunze kuhusu wajibu wa serikali kwa wananchi, kumekuwa na dhana potofu kuwa wajibu wa serikali ni kuwafanyia wananchi kazi ili wapate mafanikio katika maisha yao. Wengine huenda mbali zaidi wakisema kuwa yapasa serikali iwajengee hata nyumba. Kiukweli huu ni uongo au dhana potofu na haitakuja kutokea serikali kumfanyia mwananchi maendeleo yake binafsi, au asije akaja mwanasiasa yeyote akakuahidi kuwa atakufanyia maendeleo yako wewe kama wewe hapo utakuwa umepotea kabisa hatimae utaishia kuilaumu tu na maisha yako yatazidi kudididmia tu katika dimbwi la umaskini!
    By @zakaboyblog
Wajibu wa serikali ni kuhakikisha inatengeneza au kurahisisha upatikanaji wa maendeleo kwa wananchi unakuwa rahisi kwa kuboresha mifumo ya huduma mbalimbali ambapo mwananchi ambae atajituma sawasawa atafanikiwa kupitia huduma hizo na juhudi zake binafsi. Kama utalemaa hakika hakuna wokovu lelemama ambao utakuja ukukute umekaa.
Katika uchaguzi mkuu kila mtu anaetaka uongozi hufanya kampeni kwa kunadi sera zake ili apewe nafasi ya kuongoza nchi kwa kuboresha vipaumbele vyake kwa maslahi ya taifa na mengine aliyo na agenda nayo. Na si kweli kwamba serikali itakuja kwa Thomas Malale na kumjengea nyumba imfungulie biashara, kiukweli hicho kitu hakipo. Hebu tuangalie mifano ya huduma ambazo serikali inaweza kuzifanya na jinsi ambavyo zinaweza kukusaidia kuboresha maisha yako na kufikia mafanikio katika mtazamo sahihi na si ule wa kuletewa maendeleo hapo uliopo;
  • Huduma za jamii; hapa ebu tuangalie baadhi ya hizo huduma. Kama serikali ikiboresha barabara si kwamba wewe mwananchi utaona moja kwa moja faida yake ila kuna faida wanaziita zisizo za moja kwa moja lakini ni muhimu sana katika mafanikio ya maisha yetu. Mfano kama wewe ni mfanyabiashara na usafirishaji wa bidhaa ndio hujenga asilimia kubwa ya biashara yako barabara itakuwa msaada kwako katika kufikia mafanikio yako kwa sababu; kwanza itakuwa inarahisisha usafirishaji wa bidhaa zako; pili, itasaidia kuokoa muda ambao ungekutumika mwingi kwa usafirishaji kwenye barabara mbovu; tatu, vyombo vyako vya kusafirishia havitapata hitilafu za mara kwa mara hivyo kuokoa fedha ambazo zingetumika kufanya marekebisho na kupelekea hasara. Vivyo hivyo kwa huduma zingine kama Afya na Elimu; kama kukiwa na huduma bora za afya zitasaidia mwananchi kutatua tatizo la magonjwa ambalo ni kikwazo katika shughuli  zao za maendeleo, halihadhalika kwa elimu pia mwananchi anapopata huduma bora zinamsaidia yeye binafsi kuongeza maarifa yake yatakayo muongoza katika shughuli zake za maisha ambazo amejiwekea ili aweze kufikia mafanikio. Sasa kwa muktadha huu serikali haijakuletea maendeleo moja kwa moja nyumbani kwako bali imeboresha miundo mbinu ya wewe kufanikiwa, kazi inabaki kwako wewe mwananchi kujikwamua
  • Huduma za kiuchumi; kama tulivyoona hapo juu hata katika huduma za kiuchumi serikali haileti maendeleo nyumbani kwako bali inaboresha mazingira yawe mazuri na ya kuvutia kwa wananchi kufanya biashara au shughuli zingine za kiuchumi. Mfano kama kuna sheria ambazo ni kikwazo kwa wananchi wazawa kuanzisha labda kampuni za huduma fulani ili wananchi waweze kunufaika serikali inaweza kufanya marekebisho ya sheria hiyo au kutunga nyingine ambayo itaendana na mahitaji ya wananchi wake ili waweze kuendelea kiuchumi. Pia inaweza kuboresha mahusiano na nchi marafiki ili kusaidia upatiakanaji wa masoko kwa bidhaa zinazozalishwa na wananchi, uboreshaji wa huduma za kibenki n.k. hapa serikali itakuwa imeboresha miundo mbinu ya uchumi hivyo wewe kama mwananchi jukumu lako ni kuchangamkia fursa tu ili upate kuyaona mafanikio na si kwa kulalamika kuwa serikali haisaidii mwananchi ilihali imekwisha fanya sehemu yake.
Naomba tuishie hapo mifano ipo mingi sana lakini lengo lilikuwa kukupatia taswira ya wajibu wa serikali na jinsi gani wewe kama mwananchi unaweza kufikia mafanikio yako kupitia wajibu wake huo. Labda kwa ufupi tu ni kwamba hatima ya maisha yako unayo wewe mwenyewe aidha uamue kufanikiwa ama kushindwa vyote vinatokana na uamuzi wako wewe mwenyewe. Hakuna mtu atakaekuja kukushika mkono na kukulazimisha kufanya kazi ili ufanikiwe. Na hivyo ndivyo ilivyo hata kwa serikali haimfati kila mmoja na kumwambia imfanyie nini ila hufanya kwa ujumla wote wanufaike na wale wanaolaumu kila siku serikali na kuishia kukaa tu wataendelea kufifia kimaendeleo badala ya kuchakarika na kazi. Zinduka Mtanzania, achana na dhana potofu!
By @zakaboyblog

Jumatatu, 18 Machi 2019

FANYA HATUA HIZI UJITAMBUE ZAIDI

Tafakari yetu leo inahusu WEWE NI SEHEMU YA MFUMO
?
Karibu kila kilichoumbwa duniani ni sehemu ya kingine , kwa hiyo tuseme hata sisi binadamu ni mfumo. Lakini kabla sijaingia kwa binadamu embu tuangalie mfano rahisi wa MLANGO.


Wewe unapoutazama mlango mara nyingi unaangalia mlango kama mlango pekee lakini, mlango huo hauna maana kama hakuna kuta mbili kushoto na kulia kwake. Huo mlango pia usingekuwepo kama kusingekuwepo ardhi au sakafu hapo chini. Mlango wenyewe tuu umeundwa na vitu vingi kama kitasa au komeo, pia kulihitajika misumali n.k. Hata hivyo wewe bado unapozungumzia mlango akili yako moja kwa moja huangalia tuu Hicho ambacho sote huwa tunasema mlango ila kiukweli MLANGO ni jumla ya vyote vinavyofanya nyumba au chumba chako kijihifadhi kwa kuzuia kuingia kwa urahisi.

Wewe pia tunapokuangalia haraka haraka tunakuona wewe tuu, lakini wewe ni jumla au matokeo ya walezi wako, mke/mume wako, elimu uliyoipata, unachokula na kunywa, marafiki n.k. Ndio maana kama ukiishi eneo tofauti, ukawa na marafiki tofauti, ukapata elimu tofauti , ukawa na mpenzi/mke/mume tofauti, pengine wewe wa leo sio yule utakayekuwa wa wakati ujao.


--Kwa nini nimeleta tafakari hii ? Ni kwa sababu kama ukijitambua kuwa wewe ni sehemu ya MFUMO basi utajitahidi kuangalia namna vingine vinavyounda mfumo vinavyosababisha wewe kuwa hivyo ulivyo. 
Pengine ni aina ya mambo unayojifunza, aina ya siasa unayofuata, yale unayosoma na kuamini, pengine ni aina ya marafiki ulio nao, pengine ni mazingira unayoishi, n.k. 
Je kwa kiwango gani upo makini na kuvitumia vitu vingine au watu wengine katika mfumo wako ili uwe mtu bora zaidi ? 
Tafakari , chukua hatua ya KUJITAMBUA ZAIDI.

Jumapili, 17 Februari 2019

Susuboy classic l hello audio



                 SUSUBOY CLASSIC
                 
                       > HELLO<
                          AUDIO

       By zakaboyblog fb zakaboytz

UNAWEZAJE KUSHINDA ZAMBI KATIKA MAISHA YAKO KATIKA KRISTO


Swali: "Ninawezaje kushinda dhambi katika maisha yangu ya kikristo?"

Jibu: 
Biblia inazungumzia juu ya vitu hivi tulivyonavyo ili tushinde maisha yetu ya dhambi:

(1) Roho Mtakatifu – kipawa kimoja wapo ambacho Mungu ametupa (kanisa lake) kwa ajili ya kuwa na ushindi katika maisha ya kikristo ndani ya Roho Mtakatifu. Mungu anatofautisha mtendo ya mwili na matunda ya Roho Mtakatifu katika wagalatia 5:16-25. katika andiko hilo tunashauriwa kutembea katika uwepo wa Roho Mtakatifu. “waumini wote tayari wamejazwa na Roho Mtakatifu”,lakini hapa tunasisitizwa kupatia nafasi Roho Mtakatifu atutawale na kutuongoza. Hii ina maana ya kuwa tusikilize sauti yake tusije tukatenda mapenzi yetu wenyewe.

Tofauti ambayo Roho Mtakatifu anaweza kuifanya maishani mwa mtu ni kama ile ya Petro, kabla hajajazwa Roho Mtakatifu alimkana Yesu mara tatu, na alikuwa mbeleni ameahidi kumfuata Yesu mpaka kwenye hatari ya kifo angekufa naye. Baada ya kujazwa na Roho alizungumza waziwazi na kwa ujasiri mbele ya wayahudi juu ya mwokozi katika siku ya pentekote.

Unatembea ndani ya Roho ukiwa humzuii anapotaka kujidhihirisha (“kumzima Roho” wathesalonike wa kwanza 5:19) na una kiu ya kujazwa naye kila wakati (Waefeso 5:18-21). Je mtu hujazwaje na Roho Mtakatifu? Kwanza ni kwa mapenzi ya Mungu kama vile ilivyo katika agano la kale. Alikuwa akichagua watu Fulani, kuwajaza kwa ajili ya kutekeleza kazi ama wadhifa Fulani (Mwanzo 41: 38; Kutoka 31:3; Hesabu 24:2; Samueli wa kwanza 10:10; na kadhalika.) Ninaamini kuwa kuna ushahidi katika Waefeso 5:18-21 na Wakolosai 3:16 yakuwa Mungu huchagua kujaza wale wanaojijaza Neno la Mungu kwa kuwa kote kote ni kujazwa uwezo wa Mungu.

(2) Neno la Mungu, Biblia – Timotheo wa pili 3:16-17 inasema ya kwamba Mungu ametupa neno lake ili lituandae katika kufanya kazi njema. Linatufundisha jinsi ya kuishi na cha kuamini, linatufunulia kama tumetenda makosa na kuturudisha katika njia ya sawa. Kama waebrania 4:12 inavyosema Neno la Mungu liko hai na lina nguvu ya kupenya ndani ya nafsi zetu kung’oa lile tatizo ambalo mwanadamu hangeweza kulitatua. Mwandishi wa zaburi azungumzia uwezo wa Neno la Mungu juu ya kubadilisha maisha ya watu katika zaburi 119:9,11,105 na aya nyengine. Joshua aliambiwa siri ya kushinda adui zake (inayoashiria pia vita vyetu vya kiroho) ni kwamba asilisahau Neno la Mungu bali alitafakari usiku na mchana ili akalitimize. Haya aliyatenda, ijapokuwa maagizo yenyewe hayakuwa na uhusiano na mambo ya kivita lakini yakampa ushindi katika vita vya kuimiliki nchi ya ahadi.

Hii ni sehemu ambayo mara nyingi tunaipuuza. Tunapenda kubeba biblia tukienda kanisani ama kusoma aya za kukariri lakini hatuyatilii maanani yale tuyasomayo. Hatuyatafutii nafasi maishani mwetu kiasi cha kutubu dhambi zetu na kumtukuza Mungu kwa kipawa hiki. Tunasoma tu kiasi cha kupata mtazamo Fulani juu ya wokovu lakini hatuongezi juhudi zozote katika kutafakari kwetu mara kwa mara kiasi cha kutufanya tuwe na afya nzuri kiroho.

Ni muhimu sana kwako ufanye tabia ya kusoma neno la Mungu. Kama bado hujazoea basi Roho anakusisitiza uwe na tabia ya kulisoma Neno la Mungu. Nina kushauri uwe na kumbukumbu ya yale uliyoyasoma kwa kuyanakili kwenye daftari lako au kwenye kompyuta. Biblia ndicho kifaa Roho hutumia katika maisha yetu na maisha yaw engine (Waefeso 6:17), ikiwa ni sehemu kubwa ya silaha mojawapo ambayo Mungu hutupa ili tupigane vita vya kiroho (Waefeso 6:12-18)!

(3) Maombi – Hii pia ni njia nyengine ambayo Mungu ametupatia. Njia hii wakristo wengi huitaja tu kwa maneno lakini hawaitumii. Tuna ibada za maombi na nyakati za maombi na kadhalika lakini hatuoni manufaa ya jambo hilo sawa na kanisa la kwanza (Matendo 3:1; 4:31; 6:4; 13:1-3, na kadhalika). Paulo mara kwa mara arudia kueleza vile alikuwa akiwaombea wale aliokuwa akiwahudumia. Lakini tunapokuwa peke yetu hatuitumii njiaa hii. Mungu ametuahidi mambo mazuri ya ajabu kuhusiana na maombi (Mathayo 7:7-11; Luka 18:1-8; Yohana 6:23-27; Yohana wa kwanza 5:14-15, na kadhalika.) Paulo analiongezea mkazo tena katika mafundisho yake juu ya kujiandaa kwa ajili ya vita vya kiroho (Waefeso 6:18)!

Je, ni muhimu kiasi gani njia hii? Tunapomtazama tena Petro, tunaona maneno ya kristo aliyomwambia kabla hajamkana kule Gethsemane. Yesu alipokuwa akiomba Petro alilala. Yesu akamwambia, “Kesheni mkiomba ili msiingie majaribuni: Roho inataka lakini mwili ni dhaifu” (Mathayo 26:41). Wewe pia kama Petro unataka kufanya mema lakini huna nguvu yakutosha kufanyia hayo. Lazima tufuate mausia ya Mungu, tuendelee kumtafuta, tukibisha na kumuuliza… na atatupatia nguvu ile tuitafutayo (Mathayo 7:7 na kuendelea). Lakini lazima tuitilie mkazo njia hii maishani mwetu ndiyo tufaulu. Sisemi ya kwamba maombi ndiyo njia maalum zaidi. La sivyo. Mungu ni wakutisha. Maombi ni kukubali hali zetu za udhaifu, ukuu wa Mungu mwenye nguvu na asiyeshindwa ili tupate uwezo huo huo tuweze kuyafanya yaliyo mapenzi yake (wala si yetu) (Yohana wa kwanza 5:14-15).

(4) Kanisa – Hii ni mojawapo ya njia tunazozifumbia jicho. Yesu alipowatuma wanafunzi wake aliwatuma wawili wawili (Mathayo 10:1). Tunaposoma juu ya habari za safari za wale wamishenari katika kitabu cha matendo ya mitume, hawakuenda mmoja mmoja bali katika makundi, wawili wawili au zaidi.Yesu alisema mahali wawili au watatu wamekusanyika kwa ajili ya jina langu, nami nitakuwa katikati yao (Mathayo 18:20). Anatuamuru tusiache kukusanyana pamoja kama kawaida za watu wengine zilivyo bali tuutumie wakati wa kuwa pamoja kwetu kwa kutiana moyo katika upendo na matendo mema (Waebrania 110:24-25). Anatuagiza kutubu dhambi zetu mmoja kwa mwingine (Yakobo 5:16). Katika habari za hekima katika agano la kale tunaambiwa ya kwamba chuma hunoa chuma mwenziwe, vivyo hivyo mtu huchangamsha sura ya rafiki yake (Methali 27:17) “kamba ya nyuzi tatu haikatiki rahisi.” “kuna nguvu katika umoja wa wengi (Mhubiri 4:11-12).

Baadhi ya watu ninaowafahamu wamepata kaka na dada katika kristo wanaotangamana pamoja au kwa simu na wanaelezana vile wanaendelea na maisha ndani ya kristo na wanawajibika katika kuombeana huku wakiishi maisha sawa na Neno la Mungu. Mabadiliko mara nyingine huja haraka na wakati mwengine polepole. Lakini Mungu ametuahidi ya kwamba kadri tunavyoendelea kutumia njia hizi alizotuwekea, ndivyo atatuletea mabadiliko maishani mwetu. Vumilia ukijua ya kuwa ni mwaminifu katika ahadi zake.
By zakaboyblog
By f

Jumanne, 29 Januari 2019

NGUVU YA UMAKINI UNAVYOFUKUZA UMASKINI

Katika mojawapo ya hatua za mwanadamu kujitambua, kufahamu sheria hii ni mojawapo kati ya hatua za muhimu sana kwenye kufahamu maajabu ya ulimwengu. Uelewa wa sheria hii ni faida kubwa sana hasa kwa wanadamu wanaopenda kujifunza mengi na kuboresha maisha yao katika njia sahihi.
UMAKINI: Ni nguvu kani. Ni kama vile energy. Umakini unapelekea kukusanya ufahamu wako katika sehemu moja na kupelekea nguvu zako kukusanyika na kuweka nguvu kubwa kwa pamoja.
 Mwalimu mmoja wa ki-Asia aliwahi kusema kuwa “Umakini ni kama mwanga wa jua, unauona ni wa kawaida lakini ukiweka lensi mbinuko unaukusanya mwanga ule na kuwasha moto.”
Ni sawa na umakini. Unaweza ukawa umeshawahi kuona tamaduni za Ki-Asia mtu akiwa anajifunza wanasisitiza mtu kujifunza kwanza kuuongoza umakini. Mfano Kung-Fu mtu ili aweze kutumia nguvu ya Chi anatakiwa aweke umakini wake katika nguvu hiyo na attention yake yote iwe hapo ndipo nguvu hiyo huamka.
Hapo bado hatujaingia katika sheria hii kwa undani. Hapo nilikuwa najaribu kukuelekeza umakini ulivyo. Sheria hii kiini chake kipo hivi.  POPOTE UNAPOELEKEZA UMAKINI WAKO AU FOCUS YAKO PANAKUA. Unapoelekeza ufahamu wako katika hali fulani, mawazo fulani, ufahamu fulani, utaona ufahamu huo unakua.Umakini una nguvu kubwa sana katika ulimwengu, ukijifunza chochote kwa umakini unaweza kuwa na uwezo mkubwa sana. Mfano mzuri ni pale unapoamua kujifunza kitu kama Piano na Guitar, ukiweka akili yako hapo kwenye Piano utajikuta unaweza kupiga mzunguko ambao hata hukutegemea kama ungeweza kutengeneza.
Buddha aliwahi kusema hivi,”Chochote unachokiwekea umakini ni lazima kikue
Mfano ukiwa unanyanyua vyuma misuli itatumika sana, halafu baada ya kutumika kunyanyua vyuma hukua na kujaa. Chochote unachokitumia sana kinakua au kinaboreka ili ukitumia vizuri.
Hii sio sheria ya ufahamu tu bali hii ni sheria ya ulimwengu, ni sheria ambayo Uasili au ‘Nature’ imekua ikitumia kufanya kazi yake. Mnyama akitumia kiungo fulani sana kiungo kile kinakua na kuboreka kumsaidia akitumie vyema na kwa zaidi. Kisichowekewa mtazamo au matumizi kunapotea. Hii nisheria ya asili, na hata akili ni asili hivyo ipo mpaka kwenye fikra, mawazo au misimamo.
Mfano unaweza kukuta mtu anaamini kitu fulani, ameweka ufahamu wake wote hapo na anaamini hivyo na huwezi kumbadili hivyo. Naye anaona anachoamini ni uhalisia kabisa. Kumbe ‘reality’ yake imetokana na kujizoesha kuamini hivyo na kuelekeza ufahamu wake huko mwishowe anajikuta anaamini hivyo na yeye mwenyewe hajui hilo kwani hafahamu kuwa kuna sheria kama hii duniani.
Kufahamu ufahamu huu itakusaidia kuuliza unachokiamini. Je ni kweli ‘reality’ yako imetokana na umejizoesha kuamini hivyo au kufahamu hivyo na kupelekea wewe leo hii kuona hivyo au ni reality?
Wewe ni ufahamu wako, wewe unajitambua kupitia ufahamu wako, Hakuna kitu kingekwepo bila ufahamu. Ufahamu ni kinachouona ulimwengu. Kwa sasa ufahamu wako unategemea milango yako ya ufahamu (macho, pua, ulimi, ngozi, masikio) kuutazama ulimwengu.
Ulimwengu huu ni ulimwengu wa milango ya ufahamu. Shida unazoziona, raha unazoziona zote unazihukumu kwa kusema hiki ni shida na hiki ni raha kwa kutumia milango yako ya ufahamu na sio ufahamu wenyewe.
Ungezaliwa katika ulimwengu unaoamini maumivu ni raha ungeona ni raha kwani ufahamu wako hauna uhusiano na kitu au hali yenyewe. Ufahamu unaweza kubadilika na kupelekea hali kuonekana tofauti kwani ni ufahamu unaohukumu hali na sio hali yenyewe.
Kuelewa sheria hii utajifunza kuwa kuna umuhimu wa kuwa makini na unachokiamini, kuwa makini na kinachoendelea katika akili yako, kuwa makini na matumizi ya hisia zako, kuwa makini na kutazama mawazo yako, kuwa makini kwa kutazama imani na maamuzi yako halafu linganisha na maisha yako ya nje. Kuelewa sheria hii ni kuelewa kuwa ulimwengu wa ndani yetu unaumba ulimwengu wa nje.
Watu walioweza kujitambua na kufahamu sheria hii waliweza kujitahidi kuongoza fikra zao kwa kuumba uhalisia wao. Mtu makini ni mwenye ufahamu kuwa yeye na mchango mkubwa katika kubadili maisha yake na sio kingine. Haijalishi unaishi katika hali gani, ni kubadili mtazamo wako na KUUTAZAMA MTAZAMO WAKO.
Una maumivu kwenye bega. Unaweza ukaamua kuweka fikra yako katika kuwaza jinsi ulivyo na maumivu katika bega na kukosa raha au unaweza kuweka umakini wako kwa sehemu nyingine za mwili ambazo ni nzima na kushukuru kwa kila jambo. Lakini kuna ambao wataelekeza akili yao kwenye maumivu na wengine wanakata taamaa kabisa na kuona hatapona.
Unaweza ukahisi unaumwa ugonjwa fulani na kuona unaanza kuumwa ugonjwa huo. Upo ushahidi wa kisayansi kuwa kuna magonjwa yanachangiwa na akili. Kuna dalili nyingine zimetokana na mtu kuwaza ugonjwa sana na anaanza kuona dalili.
By ZAKABOYBLOG

Jumamosi, 26 Januari 2019

TAARIFA ZA Ommy Dimpoz ANAENDELEA...

                          UPDATES

             Ommy Dimpoz
       anaendelea vizuri, neno moja
              kwake tafadhali ❤❤❤

                  By ZAKABOYBLOG

Ijumaa, 25 Januari 2019

JAMBO HILI RISIWE KIKWAZO CHA MAFANIKIO YAKO KILA MTU ANAPITIA

Haijalishi unafanya kitu gani na una uhakika gani wa kukamilisha kitu hicho, lakini huwezi kukipata kitu hicho moja kwa moja kwa jinsi unavyotaka wewe iwe. Yapo mambo ambayo ni lazima yataingilia malengo yako hayo kwa namna moja au nyingine.
Unapojiwekea malengo, utafika wakati malengo yako yataingiliwa tu. Itafika wakati pesa ambayo ulikuwa umeitenga kwa ajili ya malengo fulani, unaweza ukashangaa umeitumia kwa dharura na kujikuta tena unaanza upya.
Lakini pia unaweza ukawa umeamua kufanya kazi fulani inayohitaji utulivu, lakini ukashangaa simu ikaita, au ukapokea dharura ya kuitwa pengine na bosi wako na miingiliano mingi kama hiyo ambayo naweza kusema haikwepiki kirahisi.
Yanapotokea mambo kama haya ambayo yanaingilia ndoto na malengo yako isifike mahali ukajikuta unakata tamaa. Unachotakiwa kuelewa ni kwamba, mwingiliano wa vitu katika malengo, ni kitu ambacho kinamtokea kila mtu na kwa wakati wake.

by ZAKABOYBLOG
Fb zakaboy tz

Mwingiliano wa mambo ukizidi, ni sumu ya mafanikio yako.
Kama ikitokea umepoteza mwelekeo na huoni tena dalili ya kufanikiwa kutokana na mambo mengi kuingilia ndoto zako, usikate tamaa, unatakiwa kurudi haraka sana na kuendelea kuifatilia ndoto yako.
Usipoteze muda wako kulalamika au kulaumu hali ambayo imekupata, badala yake tumia muda huo, kutafuta njia ambayo itakufanya uirudie ndoto yako haraka sana na sio kuipotezea kama ambavyo unataka kufanya.
Ni kawaida sana kwa mambo ambayo yanaonekana kwa macho ya kawaida hayawezekani, kuingiliwa na vitu ambavyo hukutarajia. Lakini ukikata tamaa na kusema ndio basi, uwe na uhakika utaipoteza ndoto yako.
Weka mkazo katika akili yako wa kusahau karibu kila kitu nakuamini, unaweza kuirudia ndoto yako hadi kuifanikisha, hata kama hapa kumetokea mwingiliano mkubwa sana ambao kwa uwazi umeonekana kukuvuruga na kukuchanganya kabisa.
Kuingiliana mambo ambayo hukutegemea kunapokuja kama huelewi vizuri, unaweza ukaacha kila kitu, lakini nikwambie hivi tu, kitu hiki kidogo kisiwe kizuizi kwako cha kukuzuia kufanikiwa hata kidogo.
Maisha ya mafanikio makubwa bado yanakuja kwenye maisha yako, changamoto ndogo kama hizi kwako kutokea, anza kuzichukulia kama fundisho la kukukomaza na kukupeleka kwenye mafanikio  makubwa. Jipe moyo na inawezekana.
Tunakutakia kila la kheri katika kufikia mafanikio yako makubwa

Jumapili, 25 Novemba 2018

TFF yapitisha majina ya wagombea uongozi yanga haya hapa


Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imepitisha majina ya wagombea nyadhifa mbalimbali za uongozi ndani ya klabu ya Yanga.

Nafasi hizo ni zile za Uenyekiti, Umakamu na zile za Wajumbe wa Kamati ya Utendaji.

Zoezi linalosubiriwa hivi sasa ni la mapingamizi pekee kabla ya kuelekea kwenye kampeni na baadaye uchaguzi ambao utafanyika Januari 13 2019.  By Zakaboyblog 



Ijumaa, 24 Agosti 2018

UNATAKA KUWA MTU MWENYE UELEWA MKUBWA SOMA HII

    By zakaboyblog #fb @zakaboytz


Kila mtu anaweza kuwa na uelewa (knowledge) mkubwa, na sio lazima awe msomi wa kiwango cha juu. Kuzingatia tabia hizi 10 kunaweza kumfanya mtu yeyote kuwa mwenye uelewa mkubwa

1. ‎Kusoma kila nafasi inaporuhusu - iwe ni gazeti, vitabu au yaliyomo mtandaoni. Epuka kusoma "vitu visivyo na maana" na badala yake zingatia vitu vya kukuelimisha, kukuhabarisha au hata kukuburudisha. Usipitishe siku bila kusoma kitu cha maana.

2. ‎ Kiu ya kufahamu kuhusu watu. Si kufahamu kwa minajili ya umbeya bali kwa mfano "flani aliwezaje kufikia mafanikio aliyonayo?" 

3. Kufundisha watu wengine. Kadri unavyofundisha watu wengine ndivyo kadri unavyojiimarisha katika mada unayofundisha.

4. ‎Kushiriki mijadala ya maana

5. ‎Kufanya chemshabongo (zipo nyingi tu mtandaoni) lakini pia waweza kufanya na mtu mwingine, anakuuliza maswali/mafumbo

6. ‎Kuangalia vipindi vya runinga vinavyoeleza matukio/vitu muhimu vilivyoifikisha dunia ilipo leo 

7. ‎Kutengeneza mtandao wa marafiki wenye ujuzi/utaalam katika mambo mbalimbali (networking)

8. ‎Kujifunza kuhusu vitu vya kumfanya mtu kuwa bora zaidi (self-development)

9. ‎Kutobweteka na uelewa uliopo kichwani hata kama ni mwingi. Uelewa ni chakula cha ubongo. Hakikisha huunyimi ubongo wako mlo wake

10. ‎Kujiamini.

Alhamisi, 24 Mei 2018

HASARA NA FAIDA ZA BIASHARA YAKO


https://www.facebook.com/ZAKABOYBLOG/


Umewahi kufanya biashara kisha biashara ikafa na kupata hasara? Je, uliwahi kujiuliza ni biashara imefirisika au wewe umejifirisi (umefirisi) biashara?
Mara nyingi biashara haiwezi ku collapse over night. Ni process yaani inaanza kutoa viashiria kidogo kidogo mpaka mwisho ina meet natural death.
Kwa mfanyabiashara makini ni lazima ajifunze:
1. Kuepuka viashiria vya kufilisika biashara
2. Kugundua viashiria hivyo
3. Kutafsiri viashiria hivyo.
Ni muhimu kujua kuwa viashiria vya kucollapse biashara vinatoka ndani na nje. Vishiria vya nje ni kama vile:
1.Kupungua kwa mauzo/wateja kutokana na soko kutokuwa zuri hivyo biashara kutofanya vizuri.
2.Kuongezeka kwa kodi (pango,TRA,Leseni nk) kiasi cha kufanya matumizi kuwa makubwa pengine kuliko mauzo. Hii hasa ni kwa biashara ndogo au inayoanza
Mara nyingi viashiria hivi vya nje ni rahisi kuvigundua na kuvichukulia hatua stahiki.
Sasa tuangalia viashiria vya ndani ambavyo kwa kiasi kikubwa ndivyo vinapelekea biashara kufa. Mara nyingi hivi husababishwa na mwenyebiashara. Ikumbukwe kuwa ipo tofauti kubwa kati yabiashara na mwenyebiashara. Mara nyingi mwenyebiashara anapoingilia biashara basi kuna uwezekano mkubwa wa kudorora kwa biashara na hatimae biashara kufa.
Mfano:
1. Kuikopa biashara bila mwenyebiashara kuilipa biashara. Hapa ni pale unapochukua unga, sabuni, sukari kwenye duka lako bila kulipa. Mbaya zaidi hata kuandika kuwa ulikopa huandiki kwa vile tu wewe ndie mwenye biashara.
2. Kutoweka rekodi za biashara. Mfano: kutopiga hesabu kila silu, wiki, mwezi nk. Yani unafanya tu biashara kiholela, hujui stutus ya biashara yako ikoje.
3. Kufanya matumizi yasiyo ya lazima ndani ya biashara. Mfano kuingiza mzigo mpya wakati wa zamani haujauza, unafanya hivyo ili tu shelf za duka zisionekane tupu (mbavu za mbwa), au unanunua gari la kutembelea kwa pesa ya biashara ,wakati kumbe kwa wakati huo ulitakiwa uendelee kupanda daladala kwenda kwenye biashara yako kwa sababu hali ya biashara haijawa nzuri kukuruhusu kununua gari.
4. Kutokujilipa mshahara/posho. Wewe unaihudumia biashara ,hivyo ni sehemu ya wafanyakazi wa biashara, unatakiwa ujilipe posho au mshahara kiasi utakachoamua kwa kuzingatia Hali halisi ya biashara. Wengi hawajilipi matokeo yake anaona kama hakuna faida anayopata ,hivyo anachofanya ni kudokoa kodogo kidogo kwenye mtaji akodhani ndio njia ya kujilipa kutokana na faida anayopata.
5. Kufanya biashara kimazoea! Hapa mfanyabiashara anaweza akawa anafungua au kufunga duka kwa mfano muda wowote anaojisikia, bila kujua kuwa kufanya hivyo ni kupoteza wateja. Pia kukopesha wateja kimazoea kama vile ndugu, au rafiki ambapo mwisho wa siki anashindwa kuwadai na inakuwa imekula kwake, hatimae anakuwa ameifilisi biashara.

Jumatano, 9 Mei 2018

YOUNG MASTER WATAFELI TAZAMA SIKILIZA


           YOUNG MASTER|WATAFELI
                         By Zakaboy blog

Jumatatu, 16 Aprili 2018

Dully Sykes amfunda Alikiba kuhusu maisha ya ndoa

Msanii Dully Sykes amesema Alikiba anapoingia katika maisha ya ndoa anapaswa kuelewa si jambo dogo la kuchukulia kawaida.

Muimbaji huyo ameiambia Planet Bongo, EA Radio kuwa amefurahi sana kusikia Alikiba anaoa binti kutoka Mombasa, Kenya kwani kitendo kicho kinaweza kufanya na yeye akabadili mawazo ya kuoa hapa nchini na kwenda kuoa nje.
“Mimi nampenda Ali mdogo wangu na anajua, namtakia maisha mema kwenye ndoa na namsihi ndoa si kitu kidogo, asikirie ndoa ni kitu kidogo. Anapoamua kumchukua mtoto wa watu hasa ambaye amemtoa nchi nyingine inabidi amheshimu sana, amuonyesha upendo yule mtoto,” amesema Dully Sykes.
Ameongeza kuwa mara baada ya kuona Mr. Blue ameoa amehamasika kufanya hivyo kwani ndoa hiyo imekuwa ikimvutia sana, hivyo na yeye yupo mbioni kufanya hivyo.
 By  ZAKABOYBLOG shere 

Ijumaa, 13 Aprili 2018

UKITAKA KUOA USIFANYE HAYA

MWANANGU, NAKUPENDA ILA NISIKILIZE;

1. Mwanangu, mwanamke anaweza kuwa mkeo, mwingine anaweza kuwa mama wa watoto wako, lakini ukipata mwanamke ambae atakuwa kama mama kwako, mama kwa wanao na mama kwa familia, tafadhali mwanangu usimuache huyo!

2. Mwanangu, usimfanye mwanamke wako kuwa ndio wa kupika na kufanya kazi zote za jikoni peke yake, tabia hiyo sio nzuri Kwani hata nyakati zetu, mashamba yetu yalijulikana kwa majina yetu wanaume lakini tulifanya kazi pamoja!

3. Mwanangu, nikikwambia wewe ni kichwa cha familia, simaanishi kutuna kwa pochi lako, usiangalie kabisa pochi yako, angalia kama utaona tabasamu usoni kwa mke wako. Pesa sio kila kitu katika ndoa na haileti ukuu wa familia!

4. Mwanangu, ukitaka kuwa na maisha marefu na ukapunguza misongo ya mawazo, ongea na mkeo pangeni bajeti ya mahitaji yenu, kisha mwache mkeo awe na jukumu la kuratibu mahitaji ya kila siku ya familia kwa kumkabidhi fungu husika hata kama limetokana na michango yenu wawili. Wanawake wanajua sana kupanga bajeti na hii haitakuwa rahisi kwa yeye kutumia hela hovyo wakati akijua kuwa nyumbani kuna mahitaji ya msingi, lakini hela zikiwa mikono mwako ataendelea kuomba hata kama utakuwa umeishiwa!

5. Mwanangu, Usithubutu kumpiga mkeo, maumivu ya kipigo hukaa ndani ya moyo wake kwa muda mrefu sana na huacha kidonda ambacho hukawia sana kupona. Ni hatari sana kuishi na mwanamke mwenye majeraha moyoni!

6. Mwanangu, sasa unaamua kuoa,kama bado utaendelea kuishi maisha kama ya ubachela na mke wako, sio muda mrefu utakuwa bachela tena. ukioa Badilika anza kuishi maisha ya mke na mume!

7. Mwanangu, zamani tulikuwa na wake wengi na watoto wengi kwa sababu tulikuwa na mashamba makubwa na mavuno yalikuwa makubwa, lakini kwa sasa maisha yamebadilika, kwa hiyo mkumbatie mwanamke wako peke yake kwani hakuna ardhi tena na mahitaji ya watoto ni makubwa sana. Angalia ukubwa wa familia yako!

8. Mwanangu, chini ya mwembe ambao nilikuwa nikikutana na mama yako inaweza kuwa ni hoteli kubwa kwa nyakati zenu,lakini kumbuka, kitu pekee tulichoweza kufanya chini ya mwembe ilikuwa ni kukumbatiana pekee. Nakushauri ukikutana na marafiki wa kike kikubwa unachoweza kufanya nao ni kupeana mikono na ikizidi ni kukumbatiana hadharani sio vinginevyo!

9. Mwanangu, usibadilike mara utakapoanza kupata mafanikio Zaidi, kuliko kuwahudumia hao viruka njia wa mtaani ambao hawajui mmetoka wapi na mkeo, nakushauri utumie na kufurahia mafanikio yako na mkeo ambae aliweza kusimama imara wakati wote wa mapito yenu magumu.

10. Mwanangu, kumbuka unapoanza kusema au kuona mke wako kabadilika, ujue kuwa kuna kitu ambacho ulikuwa ukikifanya umeacha kukifanya. Jitathmini na anza kufanya au kutimiza wajibu wako.

11. Mwanangu, usijaribu kumfananisha au kumlinganisha mke wako na mwanamke mwingine wa nje, kwani hata yeye anakuvumilia sana na hajakufafanisha na mwanaume mwingine yeyote huko nje na ndio maana aliamua kuwa na wewe.

12. Mwanangu, sasa hivi kuna hiki kitu kinaitwa haki za wanawake, sawa, kama mwanamke anasema ana haki sawa na wewe katika nyumba, basi gawanya mahitaji yote ya ndani kwenu katika sehemu mbili zilizo sawa, halafu timiza nusu yako na mwambie atimize nusu iliyobaki.

13. Mwanangu, nilimuoa mama yako akiwa bado kigoli(bikra) na nilikuwa naenda sana kwao kabla sijamuoa, lakini kutomkuta mkeo bikra kusikufanye umlaumu kuwa alikuwa muhuni, kumbuka wanawake wa enzi zetu na wasasa ni tofauti, ulimchagua mwenyewe na ukigoli wake hukuujua kabisa. Usiingize mambo ya kabla ya ndoa kwenye ndoa yenu.

14. Mwanangu, sikuwapeleka dada zako shule kwa kuwa nilikuwa mjinga kama wazee wengi wa hapa kijiji wasemavyo. Tafadhari usifanye ujinga huu, kwani kiwango cha mafanikio ya wanawake sasa kimefanya wanaume waonekane ni watu wa kawaida sana na sio muhimu kama enzi zetu. Ukijaliwa watoto wape elimu.

15. Mwanangu, zamani enzi za ujana wetu, wanawake walikuwa na urembo wa asili, ingawa siwezi kukudanganya, wengine waliongeza urembo kwa kujichora hina na hata kutoboa pua na masikio lakini usisahau hawakuonyesha maumbile yao nyeti hadharani kama sasa. Hakikisha mkeo analijua hili!

16. Mwanangu, mama yako na mimi hatuna hisa katika kila kitu kinachoendelea kwenye maisha yenu, jaribuni kutatua changamoto zenu wenyewe bila kila mara kuja kwetu kuomba usuluhishi. Ndoa ni pamoja na ukomavu wa kutatua changamoto zenu bila kuziuza kama gazeti kwa kila mtu.

17. Mwanangu, nilimnunulia mama yako kifaa cha kupikia vitumbua ili aanzishe mradi wa kuuza vitumbua, pia nilimsaidia kununua cherehani yake ya kwanza. Tafadhari msaidie mke wako kutimiza ndoto zake kulingana na uwezo wako kama ambavyo unahangaika kutimiza ndoto zako.

18. Mwanangu, usiache kutusaidia mimi na mama yako, utu uzima una changamoto nyingi sana na Mungu akikujalia utaziona muda ukifika. Pamoja na kutimiza majukumu yako kama baba wa familia, kumbuka pia bado tunaishi na wewe ni mtoto wetu.

19. Mwanangu, kila upatapo muda wa kusali, Sali na familia yako. Kuna kesho ambayo huijui, ongea na MUNGU wako ambae anajua kila kitu kila siku!

20. NAKUTAKIA MAISHA MEMA YA NDOA MWANANGU…. NAKUPEN