Ijumaa, 10 Novemba 2017

Kumbukumbu ya arbaini ya Imam husein yawakutanisha waislamu zaidi ya milioni 30

Zaidi ya waumini  milioni therathini  wa dini ya kiislam dhehebu la shia ithna sheria  kutoka mataifa mbalimbali yamewasili karbal nchini Iraaq katika kumbukumbu ya arbaini ya Imam husein kwa lengo la kukumbuka kifo cha imam huyo.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es salaam shekhe mkuu wa dhehebu la shia ithna sheria Ahmed Jalala amesema tukio hilo la arubaini ya Imamu HUSSEIN  ambaye ni mjuu wa Mtume  ni tukio la kawaida kwa waumini wa kiislam na wasio kuwa wa kiislam.

Jalala amebainisha mafunzo mbalimbali yatokanayo na tukio hilo ni pamoja na kuuenzi utukufu na heshma ya mwanadamu Duniani pamoja na kujenga umoja upendo amani na mshikamano Nchini.

Aidha amewataka waumini wa dini ya kiislam nma wasiokuwa waislam kuhakikisha mafunzo yanayotolewa kwa vijana kutokuwa na sifa ya ugaidi na badala yake wajikite katika kusimamia amani nchini.

Katika tukio la Arbaini ya Imamu HUSSEIN mwaka huu kauli mbiu yake ni Tusimame Kutetea haki za binaadam na kupinga ugaidi.



Hakuna maoni: