Jumatatu, 25 Desemba 2017

Nikki wa Pili azungumzia changamoto ya ajira

Rapa anayewakilisha kundi la weusi  Nikki wa pili amefunguka na kusema kuwa bado ajira kwa vijana ni changamoto kubwa licha ya kuwepo na matamko yanayosema vijana ambao hawana ajira wapo katika sekta isiyo rasmi.

Nikki wa Pili kupitia mtandao wake wa Instagram ameandika "Vijana wasio na ajira wanapewa matumaini kwa kuambiwa kuwa wao wako kwenye secta isiyo rasmi, sio kwamba hana ajira bali wako secta isiyo rasmi #uongo unapotamkwa maranyingi unaanza kuonekana kuwa ni ukweli.

Nikki wa Pili  ni msanii ambae mara nyingi amekuwa akichambua mambo mbalimbali  katika kila  nyanja kama vile siasa, uchumi, burudani afya na mengine mengi.


Hakuna maoni: