Jina la Dr. Louis Shika (900 Itapendeza) limetokea kuwa kubwa sana kwa siku za hivi karibuni, hii ni kutokana na tukio la yeye kujitokeza kwenye mnada wa kununua nyumba za Lugumi.
Kwenye mnada huo Dr Shika alishinda kununua nyumba tatu kwa jumla ya Bilioni 3 lakini alishindwa kukamilisha masharti ya mnada kwa kushindwa kulipa kiasi cha feha cha asiliami 25 papo hapo na kufanya akamatwe kupelekwa kituo cha polisi kwa maana kwamba amevuruga mnada.
Baada ya tukio hilo Dr. Shika amekuwa maarufu sana amechukua headlines kwenye media mbalimbali na hata mitandao ya kijamii,pia baadhi ya makampuni yameanza kumtumia kwenye matangazo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni