Mtwara. Mbunge wa Jimbo la Ndanda na mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kusini , Cecil Mwambe anashikiliwa na Jeshi la polisi Mkoani Mtwara.
Mwambe anaendelea na mahojiano juu ya tuhuma za kutoa maneno ya uchochezi katika mkutano wa kampeni za uchaguzi mdogo wa madiwani jana mjini Mtwara.
Mwambe aliwasili katika Ofisi Mkuu wa upelelezi makosa ya Jinai Mkoa wa Mtwara (RCO) saa 6 mchana na kutoka saa 10 na kupelekwa katika kituo cha polisi.
Akizungumza wakili wake kutoka kampuni ya uwakili ya Phoenix, Rainery Songea amesema mteja wake anatuhumiwa kutoa maneno ya uchochezi katika mkutano wa kampeni.
"Inadaiwa katika kampeni za udiwani kuna baadhi ya maneno ambayo aliyatamka yanayosababisha watu kufanya makosa, mwanzoni alihojiwa na askari wengine lakini kamanda wa polisi mkoa ameagiza ahojiwe na RCO ndio tunasubiri," amesema Wakili Songea
Akizungumza mratibu wa mahusiano na mawasiliano mkoa wa Dar es Salaam ambaye pia ni mhamasishaji, Tambwe Hiza amesema kitendo cha ofisi ya mkuu wa upelelezi mkoa kutoa dhamana na kisha RPC kuagizwa ahojiwe upya huenda ni njama za kuvuruga kampeni zao.
"Jana walimuita aje leo asubuhi amekuja, sasa kuna tatizo gani tena leo kama ana jambo lolote na yeye wasimwambie aje kesho..ndio maana tunapata wasiwasi labda kuna njama za kuvuruga kampeni zetu za kesho (Alhamisi) wilayani Ruangwa," amesema Hiza
Kamanda wa polisi mkoa wa Mtwara, DCP Lucas Mkondya alipotafutwa hakupatikana.
Mwananchi:
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni