Alhamisi, 16 Novemba 2017

Katibu Mkuu wa UN ahimiza utulivu Zimbabwe

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameomba kuwe na utulivu na kuvumiliana nchini Zimbabwe.

Msemaji wake, Farhan Haq, samesema Guterres anafuatilia kwa karibu yanayojiri Zimbabwe.

Ameongeza kuwa: "Kulindwa kwa haki za kimsingi, zikiwemo uhuru wa kujieleza na kutangamana, ni muhimu sana."

Kwa mujibu wa shirika la AFP, Bw Guterres pia amesema jumuiya ya nchi za kusini mwa Afrika, Sadc, inafanya juhudi kutanzua mzozo huo.

Hakuna maoni: