Ijumaa, 20 Oktoba 2017

''Wanawake Usukani'' wapewa sifa


Taasisi ya tiba na mifupa Muhimbili MOI imewashukuru taasisi ya Wanawake Usukani  kwa kwenda kutoa misaada mbalimbali katika kitengo hicho ambacho ni muhimu kwa jamii .

Afisa uhusiano wa taasisi hiyo Patrick Jonh amesema hayo leo jijini Dar es salaam alipotembelewa na taasisi hiyo  kwenda kuchangia damu kwa wagonjwa wanaohitaji damu, kwani katika kitengo hichi kina uhitaji mkubwa wa damu ili waweze kusaidia wagonjwa.

Kupitia mkurugenzi wa kampuni ya Wanawake Usukani Martin Gabone ambae anendesha mradi wa kuwajengea wanawake uwezo amesema kuwa wamenda kutoa misaada hiyo kwani kupita taasisi hiyo wanawake wanafursa ya kujifunza udereva hivyo ni chachu hata wao pindi watakapopata ajali waweze kusaidiwa kama leo walivyofanya wao pia iwe kioo kwa watu wengine waweze kwenda kuchangia damu na kutoa misaada.

Aidha aliongeza kuwa jamii inabidi iondokane na dhana ya kwamba wanawake hawawezi kuamua jambo, kwani sasa kuna fursa nyingi ambazo wan awake wanaweza kujikomboa kiuchumi na hata kijamii.

Hakuna maoni: