Jumamosi, 9 Desemba 2017

Breaking News: Rais Magufuli katoa msamaha kwa Babu Seya na Familia yake

December 9 2017 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli ametangaza msamaha kwa Familia ya Babu Seya, Msamaha huo ameutoa wakati wa maadhimisho ya sikukuu  ya Uhuru Mjini Dodoma Leo

”Kutokana na ibara ya 45 Katiba nimeamua kumsamehe familia ya  Nguza Viking jina lingine anaitwa Babu Seya na mwanae PapiiKocha na wao naomba kuanzia leo waachiwe huru”-Rais JPM

Mbali na Familia ya Babu Seya Rais Magufuli  ametangaza msamaha kwa wafungwa 8,157 na ambao wanatakiwa kutolewa siku ya leo ni 1,828 ikiwemo familia ya Babu Seya


Hakuna maoni: