Jumatatu, 6 Novemba 2017

Makombora ya Houthis kutoka Iran ni tishio kwa Saudi Arabia

Jeshi la ushirika linaloongozwa na Saudi Arabia nchini Yemen liafahamisha kuwa makombora  yanayotumiwa na wanamgambo wa Houthis kutoka nchini Iran ni tishio kwa Saudi Arabia.

Saudi Arabia imefahamisha kuwa kitendo hicho  cha Iran kwa wanamgambo wa Houthis  ni tishio la moja kwa moja linalolenga ardhi ya Saudi Arabia.

Tangazo lillotolewa na kituo cha habari cha Saudi Arabia limefahamisha kuuwa Riyadh inajaribu kuheshimu sheria ya kimataifa  kuiijibu serikali ya Iran kufuatia kitendo hicho.

Tangazo hilo limetolewa siku mbili baada ya kuzuia makombora yaliorushwa na kundi la Ansar Allah katika uwanja wa ndege wa Riyadh.

Hakuna maoni: