Kutokana na picha ambazo zimeanza na zinaendelea kusambaa mtandaoni zikimuonyesha Dk.Shika au Mzee wa 900 Itapendeza akiwa katika muonekano wa kipapa na huku akiwa ana kula bata na warembo, jambo linalohisiwa kuwa huwenda kukawa na video mpya ya muziki kutoka kwa msanii Dogo Janja hivyo ametumika kama muhusika mkuu.
Dk. Luis Shika amejipatia umaarufu kutokana na sakata la kuuzwa kwa nyumba za mfanyabiashara Said Lugumu, ambapo aliingilia katikwa kutaja kiwango kikubwa cha pesa ili aweze kununua nyumba hicho ila cha kushaa baada ya kuibuka mshindi hakuwa na 25% za kumfanya aweze kuwa mmiliki halali wa nyumba hizo na kufanya polisi wamkamate na kumuweka ndani ambapo alitoka baada ya siku kadhaa na kuanza kupata umaarufu mara dufu.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni