Akimkabidhi hundi hiyo Meneja wa Chapa wa kampuni hiyo,Yvonne Maruma alisema kwa mjibu wa taratibu unaofanywa na kamati ya Tuzo ya VPL iliyopo chini ya shirikisho la mpira wa miguu nchini Vodacom ikiwa kama mdhamini mkuu haina budi kutekeleza matakwa yote yale yaliyopo katika mkataba na kuweza kutoa kitita cha shilingi milioni 1/-kwa mchezaji bora wa kila mwezi ikiwa na lengo la kuwapa motisha wachezaji wote wanaoshiriki ligi kikuu,Alisema Maruma.
“Kwa mjibu wa wa kikao cha kamati ya Tuzo ya VPL imeonesha kwamba mchezaji huyu alitoa mchango mkubwa kwa singida united kupata pointi 10 katika michezo mine,ambayo timu yake ilicheza kwa mwezi huo,matokeo ambayo yaliiwezesha Singida United kutoka nafasi ya 10 katika msimamo na kupanda hadi nafasi ya nne kwa mwezi huo wa Septemba,Singida United ndiyo timu iliyokusanya alama nyingi kwa mwezi huo ukilinganisha na timu nyingine 15 zinazoshiriki ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara”,Alisema Maruma
Kwa upande wake Sharif Batambuze,aliishukuru kamati ya tuzo ya ligi na wadhamini wakuu kwa kumpatia fedha hizo na kusema atazitumia vizuri ili iwe kumbukumbu nzuri katika maisha yake kwa msimu wa 2017 Batambuze.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni