Jumatatu, 8 Januari 2018

Coutinho atua Barcelona

Usajili wakati wa dirisha kubwa majira ya joto, kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp alikuwa mkali kwa Phillipe Coutinho. Alikuwa hataki mtu amsogelee hata aje na fungu kiasi gani.

Barcelona wakasema anatania huyu, wakamletea fedha Pauni 50mil akatataa

wakapanda hadi Pauni zaidi ya 80mil akagoma, wakaenda Pauni130m akagoma na hakumruhusu.

Ilimuumiza sana Coutinho, lakini akawa na akili ya kiutu uzima, akasema siku hazigandi. Akacheza mpira na hata kufunga mabao muhimu kwa timu yake.

Waandishi wa habari hawakuacha kumchokonoa, wakamuuliza, anaona vipi hilo la kucheza na alitaka kuondoka, akasema yeye ni Liverpool na anacheza mpira Liverpool.

Alhamisi iliyopita, usiku sasa, kabla ya mechi ya Everton Kombe la FA akasema kama kucheza, atacheza mechi yake ya mwisho kisha anasepa zake Barcelona.

Barcelona wakaja jumla. Liverpool waliwapandishia dau hadi kufikia Pauni 140mil, wanaume walikuwa wamedhamiria kweli. Wakaja na kianzio cha Pauni107mil kwa ajili ya kuinasa saini yake.

Alipohojiwa juzi akiwa mwenye furaha, Coutinho alisema: “Nimeshaaga washkaji zangu, marafiki wote wanafahamu naondoka.

Coutinho alitarajiwa kutambulishwa kwenye mchezo kati ya timu yake mpya na Levante kabla ya kufanya ziara ya kwenda Falme za Kiarabu Abu Dhabi.

Kiungo Coutinho kwenda Hispania, kutamfanya kuwa mchezaji wa pili ghali baada ya Neymar lakini pia ni rekodi kwa Liverpool. Liverpool ilipoipiga Everton 2-1 Kombe la FA kwenye Uwnaja wa Anfield, Coutinho aliwekwa benchi huku Virgil van Dijk akicheza kwa mara ya kwanza baada ya kumchukua kwa Pauni75m akitokea Southampton.   

Hakuna maoni: