Jumanne, 26 Desemba 2017

Serikali yapewa ushauri na Mbunge

Serikali imeshauriwa kuboresha huduma zinazotolewa na Bima ya AFya ya Jamii NHIF ili ziendane na huduma za matibabu zinazotolewa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya NHIFí ili  kumuwezesha  Mwanachama wa bima ya AFya ya Jamii kupata matibabu sawa na Mwanachama wa NHIF

Mbunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini Oran Njeza anatoa ushauri huu  akiwa katika Hospitali Teule ya Mbalizi, ambako ametoa msaada mbalimbali kwa wagonjwa ikiwa ni kusherehekea pamoja  nao sikukuu ya Noel , akiwa ameongoza na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mbeya Jackobo Mwakasole na Uongozi Chama cha Mapinduzi Wilaya na Makanda wa chama hicho.

Muunguzi Mfawidhi wa Hospital Teule ya Mbalizi Helmath Sanga anasema katika mkesha wa sikukuu ya Noel watoto kumu wamezaliwa.

Awali Mbunge huyo akiwa na  Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Uongozi wa Wilaya na Makanda wa CCM wa mefanya usafi katika Hospital teule ya Mbalizi  na Badaye kutembelea wagonjwa na kugawa zawadi ya sikukuu ya noel ambapo baadhi ya zawadi ni sabuni, mafuta ya kupakaa, soda na  juice  lakini pia akaupongeza uongozi  wa hospitali hiyo kwa kazi nzuri wanazofanya.

Hakuna maoni: