Jumapili, 24 Desemba 2017

BREAKIG NEW: RASMI SIMBA IMEMTUPIA VIRAGO KOCHA WAKE, JOSEPH OMOG

 

Simba imevunja mkataba na Kocha Joseph Omog na sasa anaondoka zake kurejea kwao Cameroon.


Simba Sports Club
Dar es salaam
23/12/2017


      TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI*
_____________________________________


Klabu ya Simba na kocha wake mkuu Joseph Omog, wameamua kwa pamoja kuvunja mkataba baina yao kwa makubaliano maalum yanayozingatia maslahi ya pande zote mbili. 

Klabu inamshukuru kocha Omog na inamtakia kila la kheri kwenye maisha yake nje ya Simba.

Kwa wakati huu Timu yetu itakuwa chini ya kocha msaidizi Masoud Djuma na itaendelea na mazoezi kesho,na kupumzika siku ya Jumatatu kwa mapumziko ya sikukuu ya Christmas na itaingia kambini Jumanne kabla ya safari ya Mtwara,ambapo tutacheza na Timu ya Ndanda kwenye mchezo wa Ligi kuu wiki ijayo.

Pia kwa niaba ya uongozi, benchi la ufundi na wachezaji.tutumie nafasi hii kuwaomba radhi sana Wanachama na washabiki wetu kwa matokeo ya jana, sote tumeumia ila ndio mchezo wa mpira ulivyo, na tuwaombe muwe watulivu katika kipindi hiki ili tufikie malengo yetu. 

Mwisho

klabu inawatakia nyote Sikukuu njema ya Noeli na mapumziko mema ya wikiendi. 

IMETOLEWA NA.... 

Haji S MANARA
Mkuu wa Habari Simba Sc

SIMBA NGUVU MOJA


Hakuna maoni: