"maeneo ya pwani kwa magonjwa haya sio kitu cha ajabu sana hivyo kama mkoa lazima tujipange na kuweka mikakati kwa kujenga uwezo wa ndani kwa kuwahudumia wagonjwa wetu", alisema Mh, Makonda.
Mh, Makonda alitoa rai kwa watu wanaopotosha jamii kwa kusema dawa hizo zinapunguza nguvu za kiume na kwamba sio mda sahihi wa kusema hayo kwani serikali ina lengo zuri kwa wananchi wake na wanahitaji kuona wako na amani na furaha mda wote.
Aidha kwa upande wake dokta GRACE MAGEMBE amesema kuwa katika kutekeleza azima hii ya kugawa dawa za kinga tiba bure, wamepitia hatua mbalimbali kwa kutoa mafunzo, kugawa dawa kwa wilaya zote pia wanahamasisha wadau wote ambapo kesho utafanyika uzinduzi rasmi eneo la Kigambo, jijini Dar es salaam.
Kutokana na takwimu zinavyoonyesha lengo la wizara ni kuhamasisha jamii kutumia dawa hizi kama mkoa una wagonjwa wengi ambapo takribani watu 2222 wanaugua matende na 4162 wakiugua mabusha.
Pia kutokana na takwimu hizi watu wanashindwa kufanya kazi zao vizuri, kwa kutambua hilo serikali ina malengo ya kuhamasisha jamii kutumia kinga tiba ili kuondoa maradhi haya.
Kwa kuzingatia lengo la kuwafikia wananchi wote kutakuwa na vituo katika maeneo mbalimbaliu ya wazi ikiwezo vituo vya mabasi, sokoni, hospitalini, kambi za jeshi na ofisi za serikali za mitaa, hivyo wananchi wote kuanzia miaka mitano na kuendelea wajitokeze kupata kinga tiba ya mabusha, matende na minyoo ya tumbo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni