Jumapili, 26 Novemba 2017

SIMBA YAAMBULIA SARE NA LIPULI FC, HAJI MANARA AMLAUMU MWAMUZI


Ligi kuu ya Vodacom Tanzani bara imeendelea tena leo wa mchezo mmojakati ya Simba na Lipuli Fc,mchezo uliofanyika katika uwanja wa uhuru jijini Dar es salaam.

Mchezo huo umemalizika kwa timu zote kuondoka na point moja kila moja baada ya kutoka sare ya kufungana goli moja kwa moja.

Simba ilikuwa ya kwanza kupata goli katika dakika ya 15,goli liliofungwa na Mwinyi kazi moto, dakika mbili baadae Lipuli walisawazisha kupitia mchezaji wao Asante Kwazi.


Akizungumza na waandishi wa habari baada ya mchezo huo, msemaji wa timu ya Simba ,Haji manara amesema kwamba ipo haja sasa ya TFF kutoa adhabu kali ikiwemo kufungiwa kabisa  kwani wao ndio wanaovuruga michezo.

Manara amesema licha ya wachezaji wa Simba kukosa nafasi za wazi lakini mwamuzi amekuwa kikwakozo kwenye mchezo huo.

Zifuatazo ni picha mbalimbali za mchezo huo






kikosi Cha Simba kilichoanza kwenye mchezo huo

Kikosi cha Lipuli Fc kilichoanza kwenye mchezo huo


Kocha wa Lipuli Fc, Suleiman Matola



Wachezaji wa Lipuli wakipasha Viungo kabla ya Mchezo Kuanza
















Kipa wa Lipuli Fc










Shiza Kichuya akiwa chini baada ya Kuchezewa Faulo










Hakuna maoni: