Jumapili, 5 Novemba 2017

Raia wa Australia waandamana kupinga unyanyasaji wanaotendewa wakimbizi nchini Australia

Maelfu ya raia wa Australia yaandamana kupinga unyanyasaji wanaotendewa wakimbizi nchini Australia.

Waomba hifadhi  nchini Australia  katika kambi ya wakimbizi inayopatikana katika kisiwa cha Manus  Papua New Guinea  walikusanyika na kupinga unyanyasaji wanaotendewa.

Umoja wa Matifa amesema kuwa  wakimbizi katika kisiwa hicho  wapo katika hali ya dharura na wanahitaji msaada.

Wahamiaji hao wamesema kuwa wanahofia maisha yao kuondaka katika kambi waliokuwa wamezuiliwa na Australia. Kambi hiyo ilifunga Jumanne na huduma zote kufungwa.

Vyombo vya habari vimesema kuwa maji , umeme na chakula hakuna katika kambi hiyo iliofungwa na serikali ya Australia.

Tangu mwaka 2012 serikali ya Australia ilichukuwa hatua ngumu dhidi wa wahamiaji na kuwazuaia katika kisiwa cha Manus Papua New Guinea na Nauru.

Kwa mujibu wa taarifa zilzitolewa na Umoja wa Mataifa, wakimbizi 900 wamezuiliwa kama wafungwa katika kisiwa cha Manus, 12 000 katika kisiwa cha Nauru.

Hakuna maoni: