Wakati wa tukio hilo likiendelea watoto wa marehemu waliokuwa ndani ya nyumba hiyo walijitahidi kupambana kuwaokoa wazazi wao lakini walishindwa baada ya kushambuliwa na marungu.
Ndg. Ramadhani amesema wanandoa hao wakiwa wamelala usiku, kulitokea watu wasiojulikana wakipiga risasi hewani karibu na nyumba yao na kuwatishia majirani wasitoke nje.
Ramadhani amesema baada ya vitisho hivyo watu hao waliingia ndani na kuanza kuwashambulia wanandoa hao kwa mapanga.
Wakati wa tukio hilo likiendelea watoto wa marehemu waliokuwa ndani ya nyumba hiyo walijitahidi kupambana kuwaokoa wazazi wao lakini walishindwa baada ya kushambuliwa na marungu.
Mtendaji amesema majirani baada ya kusikia utulivu waliingia kwenye nyumba hiyo na kuwakuta wanandoa hao chini ya kitanda wakiwa na majeraha makubwa kwenye sehemu za uso na mikononi.
Mwenyekiti wa kitongoji cha Kasekese B , Happiness Bona amesema walipoona watu hao wakiwa kwenye hali mbaya walifanya jitihada za kuwapeleka hospitali lakini hawakufika walifia njiani.
Kamanda wa polisi mkoa wa Katavi, Kamanda Damas Nyanda amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo mpaka sasa miili ya wanandoa hao imehifadhiwa kwenye chumba cha kuhifadhi maiti katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda kwa uchunguzi zaidi.
Kamanda Nyanda amesema kwa sasa polisi wanafanya jitihada za kuwasaka wahalifu hao kwa hali na mali.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni